Zaidi ya wafungwa 200 wa kisiasa wa Venezuela waliingia kwenye mgomo wa kula siku ya Jumapili kama ishara ya kushinikisha waachiliwe huru chini ya sheria mpya ya msamaha ambayo haijumuishi wengi wao.
Wafungwa katika gereza la Rodeo I, takriban kilomita 40 (maili 25) mashariki mwa mji mkuu Caracas, walipiga kelele kwa wapendwa wao kama sehemu ya maandamano hayo.
Mgomo wa kula ulioanza Ijumaa usiku, ulikuja baada ya wafungwa kulalamika kuwa hawatafaidika na sheria hiyo kwa sababu haijumuishi kesi zinazohusisha wanajeshi, ambazo ndizo zinazozoeleka zaidi katika kituo hicho.
Hata hivyo kwa mujibuwa ndugu wa wafungwa hao, inasemekana sio wafungwa wote katika gereza hilo, walikuwa wakijiunga na mgomo wa kula.
Chanzo; Itv