Mwezi mmoja baada ya waasi wa AFC‑M23 kuondoka Uvira, makaburi manne ya halaiki yamepatikana katika eneo hilo la Kivu Kusini, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Ugunduzi huu umeibua hasira na hofu miongoni mwa wakazi, ambao wanataka maelezo thabiti kuhusu miili iliyopatikana, hasa wakati familia nyingi bado hazijui hatma ya vijana wao waliokamatwa na AFC/M23.
Witu wa kutaka uchunguzi huru dhidi ya tukio hilo wazidi kutolewa.
Chanzo; Dw