Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Vitisho vya Marekani vya kizamani

Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) limeonya kuwa inayoshikilia mpini na kuamua hatima ya vita vyovyote vitakavyoanzishwa na Marekani.

Alisema kama Marekani itaishambulia Iran, nguvu itakayotumika itaishangaza dunia na haitatajiwa kama inatoka ndani ya taifa hilo.

Msemaji wa IRGC, Brigedia Jenerali Ali-Mohammad Naeini, alisema siku ya Jumatano, kwamba shinikizo la kijeshi lilalofanywa na Marekani hakutazaa matunda.

Ofisa huyo wa jeshi, alisema majaribio ya kuitisha Iran kupitia ishara na utumaji wa ndege za kivita, pamoja na meli ya kubeba ndege ya Marekani jirani na Iran, sio jambo jipya kwani mbinu hiyo ni ya zamani inayotumiwa na Marekani.

Kwa mujibu wa kamanda huyo, kushindwa kwa haraka nguvu uasi unaoungwa mkono na Marekani nchini Iran, maofisa wa Marekani wamejaribu kuchochea mvutano na kueneza hofu ndani ya jamii ya Iran.

Wakati huo huo, Msemaji wa serikali ya Iran ameonya kwamba, jeshi la nchi hiiyo litajibu mapigo ili kutetea mamlaka ya kujitawala na uhuru wa taifa hilo.

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: