Shambulizi la droni limelenga gari lililokuwa limebeba familia zilizokimbia makazi yao katika eneo la Dubeiker katikati mwa Sudan na kuwaua takriban watu 24, wakiwemo watoto wanane.
Kundi moja la madaktari linalofuatilia hali ya vita katika eneo hilo limeripoti juu ya shambulio hilo, siku moja baada ya msafara wa shirika la Mpango wa Chakula Duniani kulengwa.
Hakukuwa na tamko la haraka kutoka kwa RSF ambayo imekuwa ikipigana na jeshi la Sudan kwa udhibiti wa nchi hiyo kwa takriban miaka mitatu.
Chanzo; Dw