Hivi karibuni Tanzania imeibuka kamata kamata ya watu na fungia ya mitandao ya kijamii kwa kile kinachoitwa matumizi mabaya ya mtandao huku Tiktok na X zamani twitter ikiwa mifano ya mitandao ya kijamii iliyofungiwa mpaka hivi sasa.
Nchi ya Tunisia, dhidi ya matumizi mabaya ya mitandao imeibua gunzo, Mwanaume mmoja aitwaye Saber Chouchane (56) amehukumuwa kifo “Kunyongwa hadi kufa” baada ya kukutwa na hatia ya kumkashifu Rais wa wa nchi yake Kais Saied, pamoja na kushambulia usalsma wataifa kupitia mitandao ya kijamii.
Ambapo mwanasheria wake amesema Saber, alikiamatwa mwaka jana kwa kuchapisha maandiko ya kumkosoa Rais Kais, kupitia mtandao wa facebook.
Hukumi hiyo inatajwa kuwa ya kipekee kwani haijawahi kutokea kwa kosa la aina hiyo.
Hukumu hiyo imeibua idadi kubwa ya wakosoaji mtandaoni nchini humo kutoka kwa wanaharakati na Raia wa Taifa hilo huku wengi wakiita ni mbinu ya kuwatisha wakosoaji wanaomkosoa Rais huku wakionya kuwa hatua hizo zinaweza kuzidisha ukandamizaji wa uhuru wa kujieleza nchini humo.
Chanzo: Tanzania Journal