Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Wanajeshi Wadaiwa Kuuana Wenyewe kwa Wenyewe Urusi

Wanajeshi wanne wa Urusi wameeleza kwa kina hali ya ukatili na mateso waliyoishuhudia katika mstari wa mbele wa vita nchini Ukraine.

Wawili kati yao walithibitishia BBC kuwa waliona wanajeshi wakipigwa risasi na kuuawa papo hapo kwa sababu ya kukataa kutekeleza amri za kijeshi.

Mmoja wao alisema kwamba alimwona mwanajeshi akiuawa kwa amri ya kamanda wake, kamanda ambaye baadaye alitunukiwa cheo cha Shujaa wa Urusi mwaka 2024.

Mwanajeshi mwingine kutoka kikosi tofauti alieleza kuwa alimwona kamanda wake akiwapiga risasi watu wanne kwa mikono yake mwenyewe.

"Niliwajua, nakumbuka mmoja wao akipaza sauti: 'Usinipige risasi, nitafanya chochote utakachosema,” alisema.

Mtu mwingine alisimulia kuwa aliona miili ya wanajeshi wenzake ishirini ikiwa imetupwa kwenye shimo baada ya "kuondolewa", neno la msimu wa kijeshi wa Urusi linalomaanisha kumuua mwanajeshi mwenzako.

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: