Ripoti mpya ya Transparency International inaonyesha kuwa juhudi za kupambana na rushwa katika nchi zilizoendelea kidemokrasia zimeanza kudhoofika, hatua inayoongeza wasiwasi kuhusu mustakabali wa uwazi wa utawala duniani.
Taasisi hiyo imetaja pia wasiwasi kuhusu mwelekeo wa Marekani na athari zinazoweza kusababishwa na kupunguzwa kwa ufadhili wake kwenye juhudi za kimataifa dhidi ya rushwa.
Katika faharasa ya Rushwa 2025, Denmark imeibuka kinara wa kupambana na rushwa, ikifuatiwa na Finland na Singapore. Sudan Kusini na Somalia ziko mkiani zikifuatiwa na Venezuela.
Chanzo; Dw