Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Bosi Awaamuru Wafanyakazi Waripoti Kazini Saa Tisa Usiku

Waziri Mkuu mpya wa Japan Sanae Takaichi wiki iliyopita aliwaamuru wafanyakazi wake kuripoti ofisini saa tisa usiku.

Katika taifa ambalo watu hufariki mara kwa mara kutokana na kufanya kazi kupita kiasi, hali inayojulikana kama karoshi  Takaichi amekiri kwamba hulala kwa takriban saa mbili pekee au ikizidi sana, hulala kwa saa nne, akisisitiza umuhimu wa nidhamu ya kazi.

Wakati akiwaamuru wafanyikazi waripoti kazini saa tisa usiku, Waziri Mkuu huyo wa Japan aliripotiwa kuhitaji kupitia nyaraka muhimu baada ya mashine ya fax nyumbani kwake kushindwa kufanya kazi.

Takaichi anajilinganisha na Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Margaret Thatcher ambaye alijulikana kwa kuwaamsha wasaidizi wake usiku wa manane  kwa mtazamo huo, Takaichi anapenda kujiona kama Iron Lady wa Japan.

Kuhusiana na mada hii: