Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa Rais wa Venezuela Nicolas Maduro na mkewe wamekamatwa na kusafirishwa nje ya nchi hiyo kufuatia mashambulizi makubwa ya kijeshi ya Marekani jijini Caracas.
Kwa mujibu wa Trump kupitia mtandao wake wa Truth Social, operesheni hiyo ilitekelezwa chini ya sheria za Marekani. Mashambulizi hayo yaliambatana na milipuko na helikopta kuruka juu ya jiji usiku wa kuamkia Jumamosi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Christopher Landau, amesema Venezuela imeingia “mapambazuko mapya” baada ya kuondolewa kwa kile alichokiita utawala wa kiimla.
Hata hivyo, Urusi imelaani vikali hatua ya Marekani, ikiitaja kuwa ni uchokozi wa kijeshi dhidi ya taifa huru.
Chanzo; Cnn