Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Urusi Yakanusha Kuwaajili Wakenya Kupigana Ukraine

Kwa mara ya kwanza baada ya wiki kadhaa, Urusi imevunja ukimya wake na kuamua kuzungumzia suala la wapiganaji wa Kiafrika katika jeshi lake nchini Ukraine.

Urusi imelaani kampeni hatari na ya kupotosha ya propaganda, kuhusu shutuma za kupanga mitandao ya uhamiaji, udanganyifu na watu kulazimishwa kupigana katika jeshi lake nchini Ukraine, bila kukana uwepo wa wageni katika safu yake.

Ikitaja shutuma zilizosambaa kwa wiki kadhaa, ubalozi wa Urusi nchini Kenya umezungumzia kampeni ya kupotosha ya propaganda bila kutaja ni nani, kwa maoni yake, anayeandaa kampeni hizo.

Imekana vikali maneno yanayoenea kuhusika kwa ubalozi na wafanyakazi wake katika mipango ya kuajiri watu. Pia inakana ushirikiano wowote na vyombo au watu binafsi ambao wangewalazimisha au kuwanasa Wakenya kwa visingizio vya uongo.

Aidha, kwa mujibu wa ripoti ya kijasusi iliyowasilishwa kwa wabunge katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki, zaidi ya Wakenya 1,000 wamesafiri kwenda Urusi na kuishia kupigana katika vita vya Urusi na Ukraine, wengi wao wakiwa hawajui hatima iliyokuwa ikiwangoja. Na kwamba idadi hii ni kubwa zaidi kuliko Wakenya 200 waliotajwa hapo awali na mamlaka.

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: