Awamu ya mwisho ya mazungumzo kati ya Urusi na Ukraine ambayo yamekuwa yakisimamiwa na Marekani kama msuluhishi mkuu, imehitimishwa leo bila ishara yoyote ya kupatikana kwa makubaliano.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa wajumbe wa pande zote, mazungumzo ya leo yaligubikwa na tofauti kubwa za misimamo.
Urusi imeendelea kusisitiza masharti ambayo Ukraine inayaona kuwa yanakiuka mamlaka na uhuru wake wa kitaifa, huku Ukraine ikisisitiza kuwa haiwezi kukubali masharti yanayohalalisha uvamizi au kupoteza maeneo yake.
Chanzo; Dw