Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) imeadhimisha mafanikio yake katika kupambana na UKIMWI, ikiwa ni mojawapo ya maeneo yanayoongoza duniani katika utoaji wa huduma za kuzuia maambukizi mapya na kupunguza vifo vinavyohusiana na UKIMWI.
Uongozi wa kikanda, kupitia Mkurugenzi wa UNFPA kwa Afrika Mashariki na Kusini, Lydia Zigomo, amesema SADC imepiga hatua kubwa kwa kupunguza maambukizi mapya na vifo, kutokana na mikakati thabiti ya uzuiaji na matibabu. Aidha, juhudi za kuweka haki za uzazi na upangaji uzazi katikati ya sera za maendeleo zinaonekana kutekelezeka vizuri.
Hata hivyo, Zigomo ametoa tahadhari kwamba mafanikio haya ni nyeti na yanaweza kuporomoka ikiwa mikakati haitaimarishwa zaidi, hasa kwa vijana, wanawake na wasichana ambao bado wanabeba mzigo mkubwa wa magonjwa haya.
Chanzo; Eatv