Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Kamanda Mkuu M23 Chupuchupu Kuuawa

Kamanda Mkuu wa M23, Sultani Makenga, amenusurika kuuawa baada ya kuondoka eneo la Rubaya dakika chache kabla ya shambulio la droni lililomuua msemaji wa kundi hilo, Willy Ngoma.

Shambulio hilo limesababisha vifo vya watu wengine tisa karibu na kitovu cha uzalishaji wa coltan kinachodhibitiwa na M23.

Wachambuzi wanasema kuuawa kwa Ngoma kunaweza kuongeza mvutano katika juhudi za upatanishi zinazoongozwa na Qatar, ambazo tayari zimekuwa zikikumbana na vizingiti.

Wakati huohuo, mapigano yanaendelea Masisi kati ya M23, jeshi la Congo na makundi ya wazalendo, huku M23 ikidai serikali “imeanzisha vita kamili” katika Kivu Kaskazini na Kusini.

 

 

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: