Mgodi umeanguka katika eneo la uchimbaji Tilwizembe, kilomita 25 kutoka Kolwezi, Mkoa wa Lualaba, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Kulingana na nyaraka kutoka Huduma ya Usaidizi, Usimamizi na Uendeshaji wa Uchimbaji Madini Madogo na ya Kiasili (SAEMAPE), ajali hiyo ilitokea takriban saa 3 asubuhi Jumamosi, ikafunika wachimbaji wadogo waliokuwa wakifanya kazi kinyume cha sheria.
Kwa sasa, idadi ya vifo imesalia 11 huku wengine 6 wakijeruhiwa.
Mabaki ya marehemu yameopolewa na kupelekwa kwenye chumba cha kuhifadhi maiti cha Lualaba-Mupandja.
Chanzo; Itv