Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Watu 25 Wafariki kwa Mafuriko Brazil

Takribani watu 25 wamepoteza maisha kufuatia mvua kubwa iliyonyesha Jumatatu jioni katika jimbo la Minas Gerais, kusini-mashariki mwa Brazil, na kusababisha mafuriko makubwa pamoja na maporomoko ya ardhi.

Kwa mujibu wa mamlaka za eneo hilo, watu 18 walifariki katika mji wa Juiz de Fora, huku wengine saba wakiripotiwa kupoteza maisha katika mji wa Ubá.

Idadi ya vifo inahofiwa kuongezeka, baada ya watu kadhaa kuripotiwa kupotea kufuatia kuporomoka kwa nyumba na majengo wakati wa mvua hiyo kubwa iliyonyesha usiku.

Mamlaka zimeendelea kutoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari na kufuata maelekezo ya usalama, huku operesheni za uokoaji zikiendelea katika maeneo yaliyoathirika zaidi.

 

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: