Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Ramaphosa Azimiwa Kipaza Sauti UN kwa Kufananisha Israel na Makaburu

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amezimiwa kipaza sauti kwenye mkutano maalumu wa kujadili umuhimu wa kuanzishwa taifa huru la Palestina, baada ya kuelekeza mashambulizi dhidi ya Israel akidai inachofanya Gaza ni mauaji ya kimbari.

Pia, alifananisha mateso ya Wapalestina wanayofanyiwa na Israel na waliyoyapata Waafrika Kusini wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi wa makaburu nchini Afrika Kusini.

Ramaposa alizimiwa kipaza sauti ghafla kwenye mkutano maalumu ulioitishwa jijini New York na mataifa ya Ufaransa na Saudi Arabia, siku moja kabla ya kufanyika mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Akihutubia mkutano huo juzi jijini New York, Ramaphosa alisema suluhisho pekee la mgogoro wa Israeli na Palestina ni mataifa mawili yanalotegemea mipaka ya mwaka 1967. Ambapo mipaka hiyo ilianzishwa kwa lengo la kuanzisha nchi mbili ya Palestina na Israel, lakini lilianzishwa taifa moja tu la Israel.

Licha ya kutaka kusitishwa mapigano, kuachiliwa kwa mateka, na kuondolewa kwa vizingiti vinavyozuia utawala wa taifa la Palestina ikijumuisha ukuta wa kutenganisha wa Israel, alilinganisha mateso ya Wapalestina na historia ya ubaguzi wa rangi ya Afrika Kusini.

Katika shambulio lake la hasira dhidi ya Israel, ghafla kipaza sauti chake kilizimwa.

 

Chanzo: Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: