Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Aliyehukumiwa Kifo Kwa Kumkosoa Rais Facebook Aachiliwa

Mahakama nchini Tunisia imemuachilia huru leo Saber Chouchane, mwanamume mwenye umri wa miaka 56, ambaye wiki iliyopita alikuwa amehukumiwa kifo kwa kuchapisha kauli za kumkosoa rais.

 

Kuachiliwa kwa Saber Chouchane kumetokea baada ya wimbi la ukosoaji wa umma na wasiwasi kuhusu haki za binadamu uliotokana na kesi hiyo.

Wakili wake, Oussama Bouthelja, amethibitisha kuachiliwa kwa mteja wake, huku nduguye Saber, Jamal Chouchane, pia amethibitisha taarifa hiyo bila kutoa maelezo zaidi.

Uamuzi wa awali wa kumhukumu kifo ulionekana kuwa wa kipekee katika historia ya Tunisia, taifa ambalo limekuwa likikabiliwa na ongezeko la vizuizi dhidi ya uhuru wa kujieleza tangu Rais Kais Saied alipojilimbikizia mamlaka makubwa mwaka 2021.

Makundi ya kijamii na wanaharakati wa kutetea haki za binadamu walielezea hukumu dhidi ya Saber kuwa ya kushangaza, na iliibua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu uhuru wa maoni na haki za raia.

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: