Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Rais wa Zamani Ufaransa Jela Miaka 5 Kisa Ufadhili wa Libya

Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana na hatia ya kula njama ya uhalifu katika kesi inayohusiana na mamilioni ya euro ya fedha haramu kutoka kwa kiongozi wa Libya marehemu Kanali Muammar Gaddafi.


Mahakama ya jinai ya Paris ilimuondolea mashtaka mengine yote, ikiwa ni pamoja na rushwa na ufadhili haramu wa kampeni.


Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kusikilizwa kwa kesi hiyo mzee huyo mwenye umri wa miaka 70, ambaye alikuwa rais wa Ufaransa kuanzia 2007 hadi 2012, aliitaja hukumu hiyo kuwa "haijazingatiautawala wa sheria".


Sarkozy, ambaye anadai kesi hiyo ina msukumo wa kisiasa, alituhumiwa kutumia fedha kutoka kwa Gaddafi kufadhili kampeni yake ya uchaguzi wa 2007.

Chanzo: Bbc

Kuhusiana na mada hii: