Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

FBI yawafuta Kazi Maofisa Waliopiga Magoti Kwenye Maandamano

Shirika la Ujasusi la Marekani FBI limewafuta kazi kundi la askari waliopigwa picha wakiwa wamepiga magoti kwenye maandamano ya kupinga mauaji ya George Floyd, vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti, wakinukuu vyanzo ambavyo havikutajwa vinafahamu suala hilo.

Inasemekana kuwa maajenti hao walipiga goti pamoja na wengine wakati wa maandamano huko Washington DC mwaka wa 2020.

Floyd, mtu mweusi, aliuawa na afisa wa polisi aliyepiga magoti kwenye shingo yake Mei mwaka huo, na hivyo kuzua gumzo duniani kote.

Kati ya maafisa 15 hadi 20 wanadhaniwa kufutwa kazi siku ya Ijumaa, ingawa idadi kamili haijulikani.

Shirikisho la maajenti wa FBI limelaani kusitishwa kazi kwao katika taarifa, likisema haki zao zimekiukwa. FBI ilikataa kuzungumzia ripoti hizo ilipofuatwa na BBC.
Wachambuzi kadhaa wa mrengo wa kulia walikuwa wamekosoa maafisa wa polisi ambao walionekana wamepiga magoti kwenye mitandao ya kijamii wakati huo.

Lakini wafuasi wao wanasema kupiga magoti ilikuwa mbinu ya kupunguza mivutano na waandamanaji, badala ya kuashiria kwamba mawakala walikubaliana na maoni yao.

Kitendo hicho kiligeuka kuwa ishara ya upinzani dhidi ya ubaguzi wa rangi, kwani picha za mtandaoni zilionesha muuaji wa Floyd, afisa wa polisi mweupe Derek Chauvin, akipiga magoti shingoni mwake huku akiwa amebanwa sakafuni kwa zaidi ya dakika tisa.

Uchunguzi rasmi uligundua Floyd alifariki kutokana na mshtuko wa moyo uliosababishwa na kubanwa kwa shingo.

Kwa sasa Chauvin anatumikia kifungo cha miaka 22 na nusu kwa mauaji ya Floyd. Kupiga goti pia kulitumika Marekani kama maandamano dhidi ya dhuluma ya rangi na ukatili wa polisi kabla ya mauaji ya Floyd, hasa na mchezaji wa zamani wa NFL Colin Kaepernick.

 

Chanzo: Bongo 5

Kuhusiana na mada hii: