Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya teknolojia ya Meta, zamani facebook, Mark Zuckerberg, amepandishwa Mahakamani jijini Los Angeles nchini Marekani, kujibu tuhuma kuhusu namna matumizi ya mtandao hasa wa Instagram, unavyoathiri afya ya akili kwa watoto na vijana nchini humo.
Zuckerberg, amejitetea kuhusu madai ya kuwa matumizi ya Instagram, kwa vijana na watoto nchini Marekani, imekuwa ikisababisha kuongezeka kwa magonjwa ya akili nchini Marekani.
Mtumiaji mmoja Mark Lanier, amekwenda Mahakamani kuishtaki kampuni hiyo baada ya matumizi ya Instagram na Youtube, kumsabababishia ugonjwa wa akili alipokuwa mdogo.
Mwanamke huyo anasema, mitandao hiyo miwili, ilimfanya kuwa na mawazo ya kujitoa uhai, lakini pia kupata msongo mkubwa wa mawazo.
Chanzo; Nipashe