Watu wasiopungua 15 wamefariki baada ya feri iliyokuwa imebeba abiria zaidi ya 350 na wafanyakazi wake kuzama kwenye maji ya pwani ya kusini mwa Ufilipino.
Wafanyakazi wa uokoaji wamewaokoa watu 316 waliokuwa ndani ya meli ya MV Trisha Kerstin 3, lakini watu 28 bado hawajulikani walipo.
Meli hiyo, ambayo ilikuwa ya mizigo na abiria, ilikuwa njiani kutoka kusini mwa nchi, Mindanao, kwenda kisiwa cha Jolo kusini-magharibi siku ya Jumatatu. Serikali inasema wanachunguza chanzo cha kuzama.
Chanzo; Eatv