Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

127 Wagundulika Kuwa na Mabusha Dar

Wanaume 127 kati ya 165 waliofanyiwa uchunguzi  wa mabusha mwezi huu jijini Dar es Salaam wamegundulika kuwa na ugonjwa huo.

Hata hivyo 27 kati ya waliogundulika kuwa na mabusha tayari wamefanyiwa upasuaji na wanaendelea vizuri.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 8, 2026 wakati wa kutangaza kambi ya uchunguzi na ufanyaji upasuaji wa mabusha bure iliyoanza Januari 5, 2026, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk Mohamed Mang'una amesema wagonjwa hao waligundulika baada ya kufanya uchunguzi katika kambi hiyo inayoendelea.

Amesema  katika kambi hiyo, watafanya  uchunguzi na upasuaji  bure hadi Januari 30, 2026.

"Baada ya muda huo, wale watakaohitaji kufanyiwa upasuaji wataendelea na utaratibu wa kuchangia kama kawaida," amesema.

Akizungumza hali ya ugonjwa huo ulivyo, amesema tatizo lipo sana katika mikoa ya ukanda wa Pwani kuanzia Mtwara.

 

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: