Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limewakamata watu wawili, Charles Oden maarufu Mwakasege (32) na Isack Charles maarufu Bebwa,wakidaiwa kuingilia mifumo ya makampuni ya kukopesha simu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, SACP Benjamin Kuzaga,amesema walikamatwa kwenye msako maalum uliofanyika Januari 27 hadi Februari 5, mwaka huu, ni wakazi wa Mbeya.
“Inadaiwa walikuwa wakibadili simu za mkopo na kuondoa mifumo ya ufuatiliaji, ili kukwepa ulipaji. Polisi walikuta wakiwa na simu mbalimbali pamoja na vifaa vya kufuta taarifa na kompyuta mpakato.
“Uchunguzi wa awali umebaini baadhi ya simu hizo ni za mkopo, huku nyingine zikiwa za wizi zimeibiwa,” amesema.
Chanzo; Nipashe