Dosari ya kisheria inayomhusisha wakili aliyesaini viapo vinavyohusu kesi iliyofunguliwa na Chama cha ACT Wazalendo kupinga hatua ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ya kuteketeza nyaraka maalumu za uchaguzi imesababisha iahirishwe.
Imeelezwa kuwa viapo hivyo vilivyowasilishwa mahakamani, wakili Usi Khamis Haji, ambaye hakuwa na leseni halali ya uwakili kwa wakati husika.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, Salma Ali Khamis, aliahirisha kutoa uamuzi wa kesi hiyo leo Febuari 10 Mahakama kuu Tunguu, hadi itakapotajwa Tena Februari 13 mwaka huu.
Katika kikao cha kesi hiyo, Mahakama ilielezwa kuwa viapo vilivyowasilishwa na upande wa walalamikaji, vilisainiwa na wakili huyo bila kuwa na sifa za kisheria, jambo lililoibua hoja nzito ya kisheria iliyolazimu Mahakama kuahirisha kesi hiyo.
Chanzo; Nipashe