Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amesema matumizi ya Akili Bandia (AI) ni miongoni mwa maendeleo ya kiteknolojia yasiyoepukika, lakini pia yanaweza kuwa chanzo kipya cha uhalifu endapo hayatadhibitiwa kwa umakini.
Akizungumza jijini Dodoma katika Kikao cha Kwanza alichofanya na Uongozi wa Juu wa Jeshi la Polisi, Maafisa na Askari, Waziri Katambi alisema Serikali imejipanga kuimarisha mifumo ya udhibiti wa uhalifu unaochochewa na maendeleo ya teknolojia.
Amesisitiza kuwa pamoja na manufaa ya AI katika kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi, ipo haja kubwa ya kuhakikisha matumizi yake hayavurugi usalama wa taifa.
Chanzo; Itv