Mahakama ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara imemuhukumu kifungo cha miaka 30 jela Zainabu Fulko Elias mwenye umri wa miaka 35 Mkazi wa Kijiji cha Nambawala Kata ya Lukuledi baada ya kupatikana na hatia ya kuhifadhi dawa za kulevya aina ya bangi zenye uzito wa gramu 93 katika Nyumba yake kwa lengo la kujipatia kipato.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Issa Suleiman amesema hayo leo February 19, 2026 wakati akitoa taarifa ya mafanikio ya Jeshi la Polisi kupitia ofisi za mashtataka na Mahakama za kisheria ya kushughulika na Watuhumiwa mbalimbali katika kesi zilizofikishwa kwenye Mamlaka hizo "Zainab alikamatwa tarehe 08.09.2025 na hukumu hiyo imetolewa tarehe 09.02.2026”
Chanzo; Millard Ayo