Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Corona Yarudi Kivingine Dalili Zaanikwa Hadharani

Ikiwa unasumbuliwa na koo linalouma sana pamoja na homa, huenda umeambukizwa mojawapo ya aina mpya za virusi vya Covid-19 vinavyoenea kwa kasi msimu huu wa vuli.

Kwa mujibu wa mamlaka za afya nchini Uingereza, aina mpya za virusi—XFG (inayojulikana pia kama Stratus) na NB.1.8.1 (ijulikanayo kama Nimbus) ndizo zinazoongoza kwa kusababisha maambukizi kwa sasa.

Wataalamu wa afya wanasema kuwa, kwa sasa, hakuna ushahidi kwamba aina hizi mpya ni hatari zaidi au husababisha madhara makubwa zaidi kiafya kuliko aina zilizopita.

Hata hivyo, mabadiliko ya kimaumbile yaliyojitokeza kwenye virusi hivi yanaweza kuongeza uwezekano wa kuambukiza kwa urahisi zaidi.

Dalili zinazojitokeza

Virusi hubadilika tabia zao kadri vinavyosambaa kutoka mtu mmoja hadi mwingine.

Mabadiliko hayo, yanapofikia kiwango fulani, husababisha kuibuka kwa “aina mpya” au variants.
Ripoti mbalimbali zinaeleza kuwa baadhi ya dalili zinazojitokeza sana katika maambukizi ya sasa ni pamoja na sauti ya kukwaruza na koo linalouma vikali kana kwamba limechomwa kwa wembe.

Hata hivyo, Covid-19 bado inaweza kusababisha dalili nyingi kama vile:

• Maumivu ya kichwa
• Kikohozi
• Pua kuziba au kutoa kamasi
• Uchovu wa mwili

Dalili hizi hufanana sana na zile za mafua ya kawaida au homa ya msimu, hivyo si rahisi kutambua tofauti bila kipimo rasmi.

Tahadhari na Ushauri wa Kiafya

Iwapo unahisi kuwa hujisikii vizuri na una dalili za Covid, ni vema kuepuka kukaribiana na watu walio katika hatari zaidi, kama wazee au watu wenye maradhi sugu.

Kukaa nyumbani inapowezekana pia kunashauriwa ili kuzuia kusambaza maambukizi zaidi.

Unapolazimika kutoka, vaa barakoa, osha mikono mara kwa mara, na tumia vitambaa safi (tishu) unapokohoa au kupiga chafya, kisha vitupe kwa usafi.

 

Chanzo: Bongo 5

Kuhusiana na mada hii: