Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Bodaboda Auawa Kikatili, Atupwa Makaburini

Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora limewakamata watu sita (6) kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya aliyekuwa dereva bodaboda Hamisi Nchambi (27), ambaye mwili wake ulikutwa Januari 14, 2026 katika makaburi ya Miemba, Kata ya Mbugani, Manispaa ya Tabora.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, ACP Constantine Mbogambi, amesema watuhumiwa walikamatwa wakiwa na pikipiki ya marehemu aina ya SINORAY, rangi nyeusi, usajili MC 945 FHY, yenye thamani ya shilingi milioni 2.7. Inadaiwa walimkodi kama abiria, kisha kumpeleka makaburini na kumuua kwa kumnyonga.

Katika tukio jingine, polisi wamewakamata watu wanne (4) waliokutwa na vifaa vya wizi vilivyoibwa katika mradi wa maji ya Ziwa Victoria, huku watuhumiwa wengine watano (5) wakikamatwa awali wakiwa na pikipiki tisa (9) zilizoibwa maeneo ya Tabora na Shinyanga.

Jeshi la Polisi limeahidi kuendelea na operesheni za kukabiliana na uhalifu na kutoa wito kwa wananchi kujihusisha na shughuli halali.

 

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: