Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Kesi ya Lissu Kusikilizwa iku 20 Mfululizo

Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa Tundu Lissu inaendelea tena leo, Jumatatu Februari 09.2026, Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam

Kesi hiyo No. 19605/2025 inayosikilizwa mbele ya jopo la Majaji watatu (3) wakiongozwa na Jaji Dastan Ndunguru, imepangwa kusikilizwa kwa muda wa siku 20 mfululizo kuanzia leo hadi Machi 06.2026

Ikumbukwe kuwa, kesi hiyo kwa sasa ipo kwenye hatua ya mashahidi wa Jamhuri kuendelea kutoa ushahidi wao Mahakamani hapo, hata hivyo mara ya mwisho kutajwa Mahakamani hapo mshtakiwa (Tundu Lissu) ambaye anajitetea mwenyewe aliwasilisha mapingamizi kadhaa ambayo bila shaka leo upande wa Jamhuri wataanza kwa kuyajibu mapingamizi hayo.

 

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: