Umoja wa Mataifa umesema raia kadhaa wameuawa katika machafuko yaliyotokea Kaskazini mwa Sudan Kusini ndani ya muda wa saa 48 zilizopita.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kwenye nchi hiyo changa duniani, UNMISS, umesema unatia wasiwasi na ongezeko la machafuko katika eneo la Abiemnom kufuatia ripoti za mauaji ya raia zilizopatikana, ambapo imesema kundi la vijana wenye silaha lilivamia makao makuu ya Kaunti ya Abiemnom, iliyo karibu na mpaka na Sudan, na kuwashambulia watu kiholela.
Chanzo; Itv