Saudi Arabia imesema imefanikiwa kudungua ndege zisizo na rubani (drones) zilizokuwa zikijaribu kushambulia kiwanda cha kusafisha mafuta cha Ras Tanura refinery asubuhi ya leo.
Kwa mujibu wa taarifa ya Saudi Arabia Defence Ministry iliyoripotiwa na wakala wa habari wa serikali wa SPA news agency, drones mbili zilizojaribu kufanya shambulio hilo zilidunguliwa na kuharibiwa.
Taarifa hiyo ilisema moto “mdogo” ulizuka kutokana na mabaki ya drones kuanguka wakati wa operesheni ya kuzidungua, huku ikiongeza kuwa hakuna raia waliopata majeraha.
Chanzo; Bongo 5