Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Dubai imetangaza kuanza kwa shughuli chache za usafirishaji kuanzia jioni leo March 02,2026 kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai (DXB) na Dubai World Central - Al Maktoum International (DWC).
Hata hivyo pamoja na safari hizo chache, Wasafiri wamepewa angalizo kutotumia Viwanja hivyo hadi wakiwa wamewasiliana moja kwa moja na Mashirika ya Ndege wanayosafiri nayo na wahakikishe pia wameambiwa muda rasmi wa kuondoka.
Hatua hii inakuja baada ya Viwanja hivyo kufungwa kwa muda kufuatia mashambulizi kutoka Iran yaliyoharibu sehemu ya miundombinu ya Airport hizo na kujeruhi baadhi ya Watu.
Chanzo; Millard Ayo