Shambulio la Israeli nchini Lebanon mapema leo limeua takriban watu 31, mamlaka nchini humo zimesema. Hayo yamechochewa na mashambulizi ya roketi kutoka kwa kundi la wanamgambo la Hezbollah linaloungwa mkono na Tehran dhidi ya Israel baada ya kuuawa kwa kiongozi mkuu wa Iran.
Jeshi la Israeli limeapa kuongeza mashambulizi yake nchini Lebanon na kulifanya kundi la Hezbollah kulipa "gharama kubwa" baada ya kufanya mashambulizi kadhaa katika vitongoji vya kusini mwa Beirut na kusini mwa Lebanon, maeneo ambayo Hezbollah ina ushawishi mkubwa.
Chanzo; Dw