Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Tiwa Savage Kakubali Uwezo wa Diamond

Mwanamuziki wa Nigeria, Tiwa Savage ametaja orodha ya wasanii watatu anaowakubali likiwemo jina la msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz.

Tiwa yupo Marekani kwenye ziara ya kutangaza albamu yake mpya iitwayo This is Personal itakayoachiwa hivi karibuni.

Akizungumza kwenye mahojiano na kituo cha redio cha Hot97 nchini Marekani, mkali huyo wa Afrobeat alitakiwa kuwataja wasanii watatu Afrika anaowakubali na wanaofanya vizuri.

Tiwa alieleza kuwa Diamond ni msanii mwenye kipaji kikubwa na anaiweka Tanzania kwenye ramani ya muziki kimataifa.

"Nampenda Diamond kutoka Tanzania ni balozi wa muziki wa Bongo, ni msanii wa kushangaza, ana kipaji kikubwa mimi na wenzangu tunajivunia kuwa mabalozi wa muziki wa Afrika," alisema mwanadada huyo.

Hii sio mara ya kwanza kwa Diamond kutajwa na wasanii wakubwa kuwa nyota anayefanya vizuri kimataifa na miongoni mwao ni Mmarekani Ciara aliyeshirikisha naye kwenye ngoma ya Low iliyotoka hivi karibuni.

Ikumbukwe Diamond na Tiwa waliwahi kufanya kazi pamoja mwaka 2017 kupitia wimbo wa Fire uliofanya vizuri na kuwa zaidi ya watazamaji milioni 12 katika mtandao wa Youtube.

 

Chanzo; Mwananchi Scoop

Kuhusiana na mada hii: