Mwanamuziki Nguli Super Star wa Bendi ya Twanga Pepeta Khaleed Chokoraa Tora Bora amekamatwa na maafisa wa Uhamiaji huko Dubai alipo kwenda Matembezini na Mke wake. Chanzo cha habari cha Bongo5 habari kimethibitisha kwamba baada tu ya kufika Dubai Airport maafisa wa uhamiaji walimtilia shaka na kumtia nguvuni hadi sasa bado ameshikiliwa na polisi wakiendelea na upekuzi juu yake …chanzo ni nini cha kukamatwa kwake bado haijajulikana.
Taarifa kamili zitakuijia kila tutakapozipata lakini hadi sasa yupo mikononi mwa maafisa wa uhamiaji wa uwanja wa ndege wa Dubai United Arab Emarates.
Habari hii imechapishwa katika ukurasa wa Bongo5.