Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Kendall Jenner Kuachana na Umaarufu

Mwanamitindo maarufu duniani, Kendall Jenner (29) ameweka wazi mpango wa kuachana na kazi yake hiyo pamoja na maisha ya umaarufu, akieleza kuwa sasa anataka kuishi maisha ya kawaida na kujikita katika shauku yake kubwa ya kubuni na kusanifu majengo.

Jenner aliyeanza kujulikana akiwa na umri wa miaka 11 kupitia kipindi cha familia yake, Keeping Up With The Kardashians, amesema licha ya familia yake kusaini mkataba mnono na kampuni ya Hulu kuendeleza reality show hiyo, yeye binafsi hajawahi kuvutiwa sana na maisha ya kuwa mbele ya kamera kila wakati.

Katika mahojiano na Jarida la Vogue wiki hii, Jenner amesema anapenda maisha ya kawaida yanayompa uhuru wa kuamka asubuhi na kuvaa nguo ya kuogelea au suruali ya mazoezi bila kupaka vipodozi usoni na kuishi maisha yake kutwa nzima akiwa hivyo.

"Naapa kwa Mungu, nitaacha kila kitu na kujikita katika kazi ya kubuni na kusanifu majengo. Sisemi hili kwa mzaha," alisema Jenner katika mahojiano hayo akiwa pamoja na Gigi Hadid, mwanamitindo na mtangazaji wa televisheni huko Marekani.

Mrembo huyo ambaye ni mtu wa 13 duniani kuwa na wafuasi (followers) wengi katika mtandao wa kijamii wa Instagram, ameongeza kuwa anaipenda zaidi hali ya maisha ya kawaida kuliko mwonekano wa kifahari kutoka tasnia ya mitindo.

"Naipenda nyumba yangu kule Los Angeles, lakini pia napenda maisha rahisi. Napenda kuamka kila asubuhi na kufanya mambo yangu kutwa nzima bila kuzuizi chochote. Nafikiria sana kuhusu maisha yajayo, lakini hujaribu kutopanga kupita kiasi kwa sababu unajua mimi ni mtu wa kupanga sana mambo," alisema Jenner.

 

Chanzo: Mwananchi Scoop

Kuhusiana na mada hii: