Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Ishowspeed Aishukuru Tanzania Ziara ya Afrika

Streamer maarufu Duniani IshowSpeed ameaga rasmi baada ya kumaliza ziara yake Barani Afrika, akitoa shukrani zake kwa mataifa 24 aliyoyatembelea pamoja na Tanzania licha ya kuwa hakuweza kufika nchini Tanzania ujumbe ambao umegusa moyo mioyo ya watu mbalimbali baada ya kufanya matangazo ya moja kwa moja (streams) katika nchi 20 nzuri za Afrika ndani ya siku 28 tu

Kitendo cha IshowSpeed kuitaja Tanzania kwenye shukrani zake imeonesha kuwa Speed ameona support kubwa ya Watanzania katika Live stream zake hasa alipotembelea Kenya ambapo aliandika rekodi kubwa zaidi ya mapokezi ya ziara yake jambo ambalo limeonesha ishara njema huwa dunia ikamshuhudia akitembelea Tanzania kwenye ziara zake za awamu ijayo.

Ziara hii ilimwezesha Speed kuonyesha sura halisi na nzuri ya bara la Afrika ambayo mara nyingi vyombo vya habari huificha mbele ya dunia sambamba na kuonesha maendeleo ambayo Afrika inayo kwasasa sambamba na kuelimisha dunia juu ya historia, tamaduni, mila na maisha ya Waafrika kwa ujumla.

 

 

Chanzo; Crown Media

Kuhusiana na mada hii: