Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Rema Avitupa Njee Vigezo vya Mwanamke Wake

Katika moja ya mahojiano aliyofanya staa wa muziki Nigeria, Rema aliweka wazi vigezo anavyotaka kwa mwanamke.

Rema alieleza kuwa ikitokea anataka mwanamke wa kutoka nae kimapenzi, atazingatia ambaye haongei sana, haposti mitandaoni na mwenye wafuasi wachache.

Rema alisema akitaka kutafuta mwanamke, lazima awe na sifa hizo kwasababu hapendi mwanamke muongeaji. Kutweet sana na kuchapisha mitandaoni.

"Sipendi wasichana wanaotweet, kuongea, kupost sana. nikitaka kudate na mwanamke nitatafuta mwenye wafuasi wachache kama 1,000 au 500. Ambaye ukurasa wake wa Instagram upo private," amesema Rema.

 

 

Chanzo; Mwananchi Scoop

Kuhusiana na mada hii: