Staa wa Rap, Kendrick Lamar ameweka rekodi mpya katika Tuzo za Grammy 2026 baada ya kuwa rapa aliyeshinda tuzo nyingi zaidi katika historia, akiwa na jumla ya tuzo 27, na kuvunja rekodi iliyokuwa inashikiliwa na Jay-Z ya tuzo 25.
Katika Tuzo za 68 za Grammy zilizotolewa jijini Los Angeles, Marekani, Kendrick alinyakua tuzo ya Albamu Bora ya Rap (Best Rap Album) kupitia albamu yake ya GNX na tuzo ya Wimbo Bora wa Mwaka (Record of the Year) kwa ngoma yake ya Luther aliyoshirikiana na SZA.
Pia aliondoka na Tuzo ya Wimbo Bora wa Rap (TV Off), Best Melodic Rap Performance kupitia Luther pamoja na Uigizaji Bora wa Rap kupitia ngoma ya Chains & Whips aliyoshirikiana na kundi la Clipse.
Chanzo; Global Publishers