Msanii wa R&B kutoka Marekani, Rotimi, ametoa tamko rasmi kuwahakikishia mashabiki wake kuwa yeye na mama wa watoto wake, Vanessa Mdee, bado wako pamoja.
Rotimi amesisitiza kuwa kauli yake ya “hatuachani” ni jibu kwa wote waliokuwa wakitilia shaka uaminifu wake baada ya kuonekana akiwa na msanii Ronisia.
Ameeleza kuwa hakuna mgogoro kati yake na Vanessa, akisisitiza kuwa familia yao ipo imara na wanazidi kujikita katika malezi ya watoto wao pamoja na safari yao ya maisha.
Chanzo; Global Publishers