Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

R Kelly Afumwa na Namba ya Mkuu wa Gereza

Muimbaji wa R&B kutoka Marekani, R. Kelly anaripotiwa kuwekwa chini ya uchunguzi katika gereza la shirikisho lililopo North Carolina baada ya kupatikana na namba ya simu ya mkuu mstaafu wa gereza hilo.

Kwa mujibu wa wakili wake, Kelly amewekwa katika hali ya kutengwa (isolation) kwa muda wote wa uchunguzi huo ukiendelea.

Hatua hiyo imechukuliwa kama sehemu ya taratibu za kiusalama za gereza na mamlaka zikichunguza namna namba hiyo ilivyopatikana na iwapo kulikuwa na ukiukwaji wa kanuni za mawasiliano kwa wafungwa.

Mpaka sasa mamlaka za gereza hazijatoa taarifa rasmi kuhusu matokeo ya awali ya uchunguzi huo.

Wakili wa msanii huyo ameeleza kuwa mteja wake anashirikiana na uchunguzi unaoendelea.

R. Kelly kwa sasa anatumikia kifungo gerezani baada ya kupatikana na hatia katika kesi za makosa ya kingono na usafirishaji haramu wa watu.

 

 

 

Chanzo; Bongo 5

Kuhusiana na mada hii: