Mwanamuziki kutoka nchini Kenya Bahati hatimaye amekutana na mwanamke anayedaiwa kuwa ni Mama yake Judith Makokha na kuchukua hatua ya kwenda kupima naye vinasaba (DNA).
Mwisho wa mwaka 2025, mwanamuziki huyo alizungumzia suala hilo baada ya mwanamke huyo kusambaa kwenye mtandao ya kijamii akidai kuwa yeye ndiye Mama yake Bahati.
Judith alitoa video iliyosambaa akimuomba Bahati msamaha kwa madai ya kumtelekeza zamani. Aliongeza kuwa miaka mingi iliyopita hakuwa na uwezo wa kifedha wa kumtunza mwanawe, na kwamba alilazimika kumwacha katika kituo cha watoto yatima.
Bahati alivutiwa na simulizi ya Judith lakini alisisitiza kuwa aliwahi kushuhudia mazishi ya Mama yake mzazi miaka iliyopita.
Bahati alikuwa na mashaka kwa sababu alikulia akijua anatoka kabila la Wakamba ilhali mwanamke huyo ni Mluhya.
Chanzo; Nipashe