Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Kusah Adai Ajakimbia Gharama Kuzindulia Ep Kijiji

Waswahili husema “mkataa kwao mtumwa”. Hivyo basi mwanamuziki wa Bongo Fleva  Kusah ameukataa utumwa baada kwenda kuzindua EP yake  ‘Bumbuli Boy’ nyumbani kwao Bumbuli mkoani Tanga.

Akizungumza na Mwananchi , Kusah amesema sababu iliyopelekea kufanya hivyo  ni kubadilisha mtazamo wa vijana waliokata tamaa.

“Mimi nimeamua kuifanya hii kitu local kabisa na iwe kijijini kwetu ili kuwapata watu wote, hata ambao nilikuwa nikiwamisi. Nimetokea, nimesoma Bumbuli najua changamoto za vijana wengi.

“Najua vitu vinavyowakumba watu wengi huku, sio tu nimekuja kufanya Ep ya Bumbuli Boy. Nimekuja kuongea na vijana kubadilisha mtazamo wao kwa sababu sisi ni kioo cha jamii muda mwingine tunavyoongea inakuwa rahisi wao kuwafikia,”amesema

Kusah amesema kuna utofauti mkubwa kati ya vijana wa kipindi chake na vijana wa sasa. Hivyo Bumbuli Boy ni kwaajili ya kuwapa hamasa na kurudi kwenye mstari. “Zamani wakati mimi nasoma tulikuwa tukitoka shuleni tunaenda mpirani au umechukua boda yako kwa hiyo tulikuwa bize sana. Lakini sasa hivi wanakunywa pombe, wala hawana watu wa kuwahamasisha,” amesema Kusah.

 

Chanzo; Mwananchi Scoop

Kuhusiana na mada hii: