Rapper Chidi Benz ameithibitishia AyoTV na @millardayo kwamba ni kweli Mama yake Mzazi amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Dar es salaam.
Benz amesema baada ya kuugua kwa muda mrefu, Mama yake amefariki usiku wa kuamkia leo ambapo msiba upo Nyumbani kwake Chanika.
"Mama amefariki usiku, mimi mwenyewe nilikuwa studio jana usiku kwa S2kzy, hapa tupo njiani nataka nifike Nyumbani nimuulize Kaka yangu zaidi, yeye ndio kaka yangu Mkubwa, nitawaambia baadae kuhusu taratibu za mazishi” Chidi
Chanzo; Millard Ayo