Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Yanga, Simba Kwenye Mawindo Ligi Kuu Tanzania Bara

Vigogo wa soka nchini, Simba na Yanga, leo watashuka katika viwanja tofauti nchini kuendelea na mbio za kusaka ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Timu hizo zote zitakuwa ugenini zikicheza mechi zao za viporo ambazo ziliahirishwa huko nyuma kutokana na kushiriki mashindano ya kimataifa ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga itakuwa ugenini kwenye Uwanja wa Majaliwa, mkoani Lindi kucheza dhidi ya wenyeji Namungo huku Simba ikiwa jijini Dodoma kucheza na Maafande wa Tanzania Prisons.

Namungo itakuwa inamaliza mechi zake za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ikifikisha michezo wa 15 wakati kwa upande wa mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Yanga, utakuwa mchezo wanane.

Mabingwa hao wanaingia uwanjani wakiwa nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo wakikusanya pointi zao 22, huku Namungo ikiwa nafasi ya tano, na pointi zake 20.

 

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: