Klabu ya Benfica imepanga kukata rufaa UEFA baada ya kumfungia mchezaji wao Gianluca Prestianni kufuatia tuhuma za ubaguzi wa Rangi dhidi ya mchezaji wa Real Madrid Vinicius JR.
"Klabu inajuta kunyang'anywa mchezaji huyo wakati mchakato bado unaendelea na itakata rufaa kwa uamuzi huu wa UEFA" - Uongozi wa Benfica
Hii leo UEFA imemsimamisha Kiungo wa Benfica Gianluca Prestianni kwa mchezo mmoja dhidi ya Real Madrid kupisha uchunguzi wa kesi ya ubaguzi wa rangi dhidi ya Vinicius Jr katika mchezo wa awamu ya kwanza wa "Playoff" ya UEFA CL
Chanzo; Eatv