MWAKA 1986 Simba SC ilifanya uchaguzi mkuu uliowaweka madarakani viongozi wapya, Mwenyekiti Emmanuel Makaidi na Katibu Mkuu Jimmy David Ngonya.
Wakati huo katibu mkuu anachaguliwa na wanachama, hivyo anakuwa na nguvu za kisiasa...Ngonya alikuwa na nguvu kwelikweli hadi akabatizwa jina la utani la Gorbachev, akifananishwa na Rais wa Urusi wa wakati ule, Mikhail Gorbachev.
Lakini bahati mbaya kwao ni kwamba uongozi wao ulikumbwa na ukosefu wa amani klabuni na kusababisha timu kuyumba sana.
Simba ikanusurika kushuka daraja siku ya mwisho ya msimu, kwa misimu mitatu mfululizo ambayo Ngonya na Makaidi walikuwa viongozi.
Misimu hiyo ni 1987, 1988 na 1989. Itakumbukwa kwamba wakati ule msimu ulienda sambamba na kalenda ya kawaida ya mwaka, yaani kuanzia Januari hadi Desemba.
1987
Baada ya kuwa na msimu mbaya, Simba iliingia siku ya mwisho ikiwa ya mwisho kwenye msimamo.
Mechi yao ya mwisho ilikuwa dhidi ya mabingwa watetezi, Tukuyu Stars ya Mbeya.
Mechi ikaisha kwa sare ya 5-5, Simba kunusurika kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Japo waziri wa michezo wakati huo, Fatma Said Ally, alifuta matokeo haya, na mengine mengi siku hiyo kwa viashiria vya upangaji matokeo...ila Simba ikakwepa aibu ya kushuka daraja.
Chanzo; Mwanaspoti