Winga wa Real Madrid, Rodrygo, ameonyesha kuwa tayari kuelekea mchezo wa El Clásico dhidi ya wapinzani wao, FC Barcelona, utakaopigwa Oktoba 26, 2025 kwenye Uwanja wa Santiago Bernabéu. Hii itakuwa mara ya kwanza kwa timu hizi kukutana msimu huu wa Ligi ya LaLiga.
Msimu uliopita, Barcelona chini ya kocha Hansi Flick iliibuka na ushindi katika mechi zote mbili dhidi ya Real Madrid. Timu hizo zilikutana mara nne katika mashindano tofauti, na kila mara Barcelona iliibuka kidedea.
Akizungumza na gazeti la Diario AS, Rodrygo amekiri kuwa, Real Madrid ilipata wakati mgumu dhidi ya Barca msimu uliopita, lakini amesisitiza kuwa kikosi chao kiko tayari kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha wanashinda mbele ya mashabiki wao katika uwanja wa Santiago Bernabéu.
Chanzo: Mwanaspoti