Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Simba Kumkosa Wiki 10

Klabu ya Simba Sc imethibitisha kuwa golikipa Moussa Pinpin Camara ambaye kwa sasa yupo Nchini Morocco kwa matibabu ataendelea kuwa nje ya uwanja kwa muda wa Wiki 10 huku beki Abdulrazack Hamza ambaye na yeye anasafiri kwenda Morocco anaendelea na matibabu.

Hayo yameelezwa na Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ahmed Ally wakati akizungumza na waandishi wa Habari kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Simba Sc dhidi ya Petro Atletico ya Angola utakaopigwa Jumapili Novemba 23, 2025.

“Mchezo wa Jumapili tutamkosa Moussa Camara ambaye yupo nchini Morocco alipokwenda kufanyiwa matibabu lakini pia tutamkosa beki wetu Abdulrazack Hamza ambaye na yeye anasafiri kwenda Morocco kwa matibabu zaidi. Taarifa njema ni kuwa Mohamed Bajaber amepona na hata mchezo wa kirafiki dhidi ya JKT Tanzania alianza na kucheza dakika 30".

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: