Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Scott Atamani Kumsaidia Ronaldo Kiakili

Kocha wa masumbwi Malik Scott, ameweka wazi namna anavyoweza kumsaidia mshambuliaji wa Al Nassr ya Saudi Arabia na timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo, kuboresha hali yake ya kiakili katika hatua hii ya mwisho ya soka lake.

Scott ambaye alifunga ndoa na mtangazaji maarufu wa CBS Sports Kate Abdo mnamo Septemba 2024, ameweka wazi mpango huo, akimaanisha hitaji la kumsaidia Ronaldo ambaye bado anapendwa na mashabiki wake ulimwenguni kote.
Akiwa katika mahojiano na Canada Casino, Kocha huyo mwenye umri wa miaka 44, amesema angefurahia kufanya mazungumzo ya kina na Ronaldo kuhusu maisha ya ushindani wa kiwango cha juu.

Ameongeza kuwa anafahamu changamoto za kiakili zinazowakumba wanamichezo wa kiwango cha dunia, na anaamini anaweza kuongeza kitu kwenye uwezo wa kiakili wa Ronaldo.

 

Chanzo: Mwanaspoti

Kuhusiana na mada hii: